MWALIMU AUA MWALIMU MWENZAKE KISA SHILINGI ELFU MOJA YA BILI YA UMEME




JESHI la Polisi Mkoani Dodoma linamshikilia Mwalimu wa Shule ya Sekondari ya Hombolo Justus Jackson (28) kwa tuhuma ya kumuua mwalimu mwenzie kwa kukataa kulipa sh. 1,000 ya bili ya umeme aliyo takiwa kuchangia marehemu.


Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, David Missime amemtaja mwalimu aliyeuawa kuwa ni Fredy Ndahani (29) mwalimu wa shule ya Hombolo.

Misime amesema walimu hao wote wawili walikuwa wakiishi katika nyumba moja na walikuwa wakichangia bili ya umeme katika nyumba hiyo.

Amesema katika mabishano walimu hao waliingia katika ugomvi na hivyo Fredy alisukumwa katika ukuta na kupoteza maisha papo hapo.

Kwa mujibu wa Misime Mtuhumiwa huyo ameshakamatwa na anatarajiwa kufikishwa mahakamani mara baada ya kukamilika kwa upelelezi.


 kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapowekwa kwenye mtandao huu.BOFYA HAPA

Related

KITAIFA 7938672568249396814

Asia - Leo

MZIWANDA - MSONDO NGOMA

TONBOY

TONBOY

CONTACT

Melck Studio
Tel : +25578920034
+255757605268
E-mail : melckstudio@gmail.com

SHOW LOVE TO THIS

Hot in week

Recent

Comments

Visitors


web stats
item