NEYMAR AKUTANA NA KOLOMBIA

NEYMAR AKUTANA NA KOLOMBIA
 
 Neymar Junior
FORTALEZA, Brazil
STAA wa timu ya Taifa ya Brazil, Neymar Junior, ataichezea nchi yake katika mchezo wa robo fainali dhidi ya Colombia ambao utachezwa kwenye uwanja wa Estadio Castelao mjini Fortaleza.
Neymar alizua hofu kucheza pambano hilo baada ya kupata maumivu ya goti kwenye mchezo wa raundi ya pili dhidi ya Chile.


Kwa mujibu wa daktari wa Shirikisho la soka nchini humo (CBF), Jose Luiz Runco alisema kuwa Neymar atakuwa imara kiafya hivyo yupo tayari kwa mchezo dhidi ya Colombia mjini Fortaleza.
Kocha wa Brazil, Luiz Felipe Scolari alipata wasiwasi juu ya afya ya nyota wake kutokana na mchezo mbaya aliochezewa na Chile.
Baada ya mchezo dhidi ya Chile, Neymar anadaiwa kulalamikia maumivu ya paja la mguu wa kushoto.
“Ni maumivu yake ndiyo kitu kinchotuumiza. Atapumzishwa kwenye mazoezi lakini daktari Runco amesema hakuna sababu za kuhofia kwani atamudu kucheza mechi dhidi ya Colombia,” alisema Rodrigo Paiva msemaji wa CBF.

Related

MICHEZO 275878453820421034

Asia - Leo

MZIWANDA - MSONDO NGOMA

TONBOY

TONBOY

CONTACT

Melck Studio
Tel : +25578920034
+255757605268
E-mail : melckstudio@gmail.com

SHOW LOVE TO THIS

Hot in week

Recent

Comments

Visitors


web stats
item