Obama atetea Marekani kushambulia ISIS

Wayazidi wakikimbilia Irbil, mji mkuu wa jimbo la Wakurd, kaskazini mwa Iraq
Rais Obama amesema hataruhusu wapiganaji wa siasa kali wa madhehebu ya Sunni kuunda himaya yao nchini Syria na Iraq; na ndege za Marekani zitafanya mashambulio zaidi ikihitajika.
Rais Obama aliliambia gazeti la New York Times, ni masilahi ya Marekani kuwazuwia wapiganaji wa ISIS wasisonge mbele na piya ina wajibu kuzuwia mauaji ya kimbari.
Katika hotuba yake ya kila juma, alisema wapiganaji hao wanawateka wanawake na kuwafanya watumwa wao na wanatishia kuiangamiza jamii ya madhehebu ya Yazidi yenye waumini wachache.
Alisema mashambulio ya ndege yanaweza kumaliza kuzingirwa kwa wakimbizi wa Yazidi waliokimbilia milimani.
Ndege za Marekani kwa mara ya pili zimedondosha msaada wa dharura kwa maelfu ya wakimbizi wa madhehebu ya Yazidi ambao wamenasa mlimani, kaskazini mwa Iraq.
Walikimbia makwao wakati wapiganaji wa ISIS walipokaribia.

Chanzo bbc
kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu.LIKE HAPA
 

Related

KIMATAIFA 8124286692456700111

Asia - Leo

MZIWANDA - MSONDO NGOMA

TONBOY

TONBOY

CONTACT

Melck Studio
Tel : +25578920034
+255757605268
E-mail : melckstudio@gmail.com

SHOW LOVE TO THIS

Hot in week

Recent

Comments

Visitors


web stats
item