WATU 17 WA FAMILIA MOJA WAFARIKI GAZA

http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/07/12/140712113045_gaza_512x288_bbc_nocredit.jpg

Maafisa wa Palestina wanasema kuwa watu kumi na saba wa familia moja wameuawa baada ya makombora ya Israel kuharibu nyumba moja ya ghorofa tatu ya mkuu wa polisi wa Hamas.
Tayseer Al-Batsh anadaiwa kujeruhiwa katika shambulizi hilo.
Mashambulizi hayo yanajiri baada ya wapiganaji wa Hamas kurusha makombora ya masafa marefu katika miji ya Israel ikiwemo Tel Aviv.
Maafisa wa Israel wanasema kuwa makombora mawili ya Roketi yalirushwa kutoka lebanon lakini yakaanguka katika eneo lililo wazi kazkazini mwa Israeli.
Na katika hatua ya kulipiza kisasi ,Israel ilirusha makombora nchini Lebanon na kuzidisha hofu kwamba huenda mzozo huo ukapanuka.
Takriban raia 150 wa Palestina wameuawa katika mashambulizi hayo huku ikiwa hakuna vifo vyovyote vilivyoripotiwa nchini Israel.
 kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapowekwa kwenye mtandao huu.LIKE HAPA

Related

KIMATAIFA 4745335891129659631

Asia - Leo

MZIWANDA - MSONDO NGOMA

TONBOY

TONBOY

CONTACT

Melck Studio
Tel : +25578920034
+255757605268
E-mail : melckstudio@gmail.com

SHOW LOVE TO THIS

Hot in week

Recent

Comments

Visitors


web stats
item