MAJONZI: MUIMBAJI MWINGINE WA INJILI AFARIKI DUNIA



Zikiwa ni takribani wiki tatu tangu tasnia ya muziki wa injili nchini kumpoteza mmoja wa waimbaji wake marehemu mchungaji Debora Saidi, taarifa ambazo GK imezipata ni kwamba mwimbaji mwingine wa muziki wa injili Orida Njole amefariki dunia mchana wa leo katika hospitali ya Temeke jijini Dar es salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.


Orida ambaye mpaka umauti unamfika mchana wa leo ilikuwa bado haijajulikana nini hasa kinamsumbua lakini alikuwa ameishiwa damu sana, mpaka umauti unamkuta alikuwa anatamba na album yake iitwayo 'Duniani tu wapitaji' huku kwa mujibu wa watu waliomfahamu marehemu wameeleza kwamba alikuwa mtu mchangamfu wakati wote wakati wa uhai wake na kwamba wamepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo chake.

Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina la Bwana libarikiwe!



Picha ya mbele ya álbum ya marehemu Orida Njole.


 
Marehemu Orida akiwa na mtoto yatima katika kituo cha Tosamaganga Iringa alipotembelea kituoni hapo
 kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapowekwa kwenye mtandao huu.LIKE HAPA

Related

MATUKIO 7124604959676387652

Asia - Leo

MZIWANDA - MSONDO NGOMA

TONBOY

TONBOY

CONTACT

Melck Studio
Tel : +25578920034
+255757605268
E-mail : melckstudio@gmail.com

SHOW LOVE TO THIS

Hot in week

Recent

Comments

Visitors


web stats
item