Israel,Hamas kusitisha mapigano saa 72

 

Marekani na Umoja wa mataifa wamesema Israel na Hamas wamekubaliana kusitisha mapigano kwa saa 72 katika Gaza kuanzia alfajiri leo Ijumaa.
Taarifa ya wizara Ya afya ya Gaza,tangu kuanza kwa mapigano julai 8 wapalestina 1,422 wameshauawa wengi wao wakiwa raia.
Israel nayo imepoteza wanajeshi 56 na raia wawili.
Israel inasema operesheni yake ndani ya Gaza imeundwa ili kuwalinda watu wake na mashambulizi ya majeshi ya Palestina.
Katika tamko la pamoja, Waziri wa mambo ya nje wa marekani John Kerry na Katibu Mkuu wa umoja wa mataifa Ban Ki Moon wamesema wakati huu wa usitishaji mapigano kwa saa 72 vikosi vitabakia katika eneo hilo na wakazitaka pande zote mbili kutulia bila kuyavunja makubaliano hayo lengo likiwa kuwapa nafasi wananchi wasio na hatia kutafuta maeneo ya kukimbilia kuzikwepa ghasia.
Karibia robo ya wakazi wa Gaza wamejikuta nje ya maeneo yao kutokana na ghasia hizo.

kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapowekwa kwenye mtandao huu.LIKE HAPA

Related

KIMATAIFA 8162476827714687901

Asia - Leo

MZIWANDA - MSONDO NGOMA

TONBOY

TONBOY

CONTACT

Melck Studio
Tel : +25578920034
+255757605268
E-mail : melckstudio@gmail.com

SHOW LOVE TO THIS

Hot in week

Recent

Comments

Visitors


web stats
item