MAHAKAMA YA KIKATIBA UGANDA YAFUTA SHERIA DHIDI YA USHOGA
http://melckstudio.blogspot.com/2014/08/mahakama-ya-kikatiba-uganda-yafuta.html
Mahakama ya kikatiba nchini
Uganda imefutilia mbali sheria dhidi ya wapenzi wa jinsia moja ambayo
ilisababisha mataifa ya magharibi kuinyima msaada.
Kadhalika sheria hiyo ilizua gumzo sana sio tu Uganda bali kote duniani ambapo mataifa ya Magharibi yalilazimika kuingilia kati.
Mahakama ilisema kuwa mswada huo kabla ya kuidhinishwa kuwa sheria ulipitishwa na wabunge ambao idadi yao haikutosha kupitisha mswada na kwa hivyo ni kinyume na sheria.
Vitendo vya mapenzi ya jinsia moja, tayari
vilikuwa vimeharamishwa Uganda , lakini sheria hiyo mpya pia
iliharamisha hatua zozote za kueneza mapenzi ya jinsia moja na wakati
huu hata kuwajumuisha wanawake wasagaji kama sehemu ya wapenzi wa jinsia
moja.
Mataifa kadhaa ya Magharibi yamesitisha msaada kwa Uganda hasa baada ya sheria hiyo mpya kupitishwa.
Chanzo BBC
kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapowekwa kwenye mtandao huu.LIKE HAPA

Wanaume wanaounga mkono mapenzi ya jinsia moja Uganda
Kadhalika sheria hiyo ilizua gumzo sana sio tu Uganda bali kote duniani ambapo mataifa ya Magharibi yalilazimika kuingilia kati.
Mahakama ilisema kuwa mswada huo kabla ya kuidhinishwa kuwa sheria ulipitishwa na wabunge ambao idadi yao haikutosha kupitisha mswada na kwa hivyo ni kinyume na sheria.

Baadhi ya waandamanaji waliounga mkono serikali kwa kuharamisha mapenzi ya jinsia moja
Mataifa kadhaa ya Magharibi yamesitisha msaada kwa Uganda hasa baada ya sheria hiyo mpya kupitishwa.
Chanzo BBC
kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapowekwa kwenye mtandao huu.LIKE HAPA