Mtu mmoja afa papo hapo baada ya lori kuparamia makazi ya watu na kupinduka jijini Mbeya.

Mtu mmoja amekufa papo hapo baada ya lori la kampuni ya kichina inayojenga barabara kuu ya Mbeya – Chunya kufeli breki zake likiwa kwenye mteremko mkali wa Isanga jijini Mbeya kisha kuparamia ukuta wa uzio wa nyumba ya makazi ya watu kabla ya kugonga nguzo ya umeme na kupinduka.
Ajali hiyo ambayo imetokea majira ya saa tatu asubuhi imehusisha lori la kampuni ya kichina inayojenga barabara kuu ya Mbeya – Chunya ambalo namba zake zimeng’olewa na wafanyakazi wa kampuni hiyo punde tu baada ya ajali kutokea, lakini mashuhuda wa ajali hiyo wamesema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni breki za lori hilo kukatika likiwa kwenye mteremko mkali hali iliyosababisha kupoteza mwelekeo na kuingia kwenye makazi ya watu.
Wamiliki wa nyumba ambayo imeparamiwa na lori hilo, Emmanuel John Sangu na mkewe Monica Sangu wamesema kuwa kitendo cha lori hilo kuparamia nyumba yao kilihatarisha maisha yao na familia yao na kuwa ingawa wamenusurika wamepata hasara ya kuvunjiwa ukuta wa uzio wa nyumba yao.
Jeshi la polisi mkoani Mbeya limethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa mtu aliyepoteza maisha alikuwa ni dereva wa lori hilo ambaye jina lake bado halijafahamika.
Chanzo ITV
 kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu.LIKE HAPA

Related

MATUKIO 7407758152469140030

Asia - Leo

MZIWANDA - MSONDO NGOMA

TONBOY

TONBOY

CONTACT

Melck Studio
Tel : +25578920034
+255757605268
E-mail : melckstudio@gmail.com

SHOW LOVE TO THIS

Hot in week

Recent

Comments

Visitors


web stats
item