Serena Williams bingwa US Open
http://melckstudio.blogspot.com/2014/09/serena-williams-bingwa-us-open.html

Williams ameshinda katika mchezo uliofanyika usiku wa kuamkia leo baada ya kumtwanga Caroline Wozniacki wa Denmark kwa ushindi wa moja kwa moja.
Mpambano huo wa fainali ulipigwa mjini New York ambapo Serena ameshinda kwa seti 6-3, 6-3 na kujinyakulia ubingwa huo kwa mara ya 6.
Kwa sasa Serena ndiye mchezaji nambari 1 duniani kwa mchezo huo na pia bingwa mara 18 wa Grand Slam, amekuwa bingwa wa kombe hilo mara tatu mfululizo tangu mwaka 2012.