NEWZ - T.I ASHITAKIWA KWA WIZI

  T.I ashitakiwa kwa wizi wa vifaa vya jukwaani
Rapper T.I anakabiriwa na kesi ya wizi wa vifaa vya jukwaani ambavyo alivikodi mwaka jana wakati wa Tour ya America’s Most Wanted aliyofaya na Lil Wayne na rappers wengine.
Kwa mujibu waTMZ, kampuni iliyomkodishia vifaa hivyo imeeleza katika shitaka lake kuwa ilimkodishia vifaa T.I na akalipia gharama za kukodisha lakini wakati wa kurudisha hakurudisha Screen ya gharama kubwa  inayofahamika kama Roll Drop inayotumika kuonesha picha na video wakati wa show.
Screen hiyo imetajwa kuwa na thamani ya $50,000 lakini kampuni hiyo inataka T.I ailipe $100,000 kwa kuwa katika muda wote iliyopotea ingekuwa imewaingizia kiasi hicho cha pesa kwa kuwakodishia watu wengine.
Tuhuma hizo zinakuja wakati ambapo T.I anaendelea kupiga kazi ya kuandaa albam yake mpya inayoitwa ‘Paperwork: The Motion Picture.
T.I ameeleza katika mahojiano alioyofanya hivi karibuni kuwa albam hiyo itawashikirisha Rick Ross, The Dream, Lil Boosie, Young Jeezy na wengine wengi.
Bado tarehe rasmi ya kutoka haijapangwa.

CHANZO TIMES FM

kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu.LIKE HAPA

Related

BURUDANI 4294508723930150885

Asia - Leo

MZIWANDA - MSONDO NGOMA

TONBOY

TONBOY

CONTACT

Melck Studio
Tel : +25578920034
+255757605268
E-mail : melckstudio@gmail.com

SHOW LOVE TO THIS

Hot in week

Recent

Comments

Visitors


web stats
item