Snoop Dogg aigomea show akitaka promota atume 'private plane'
http://melckstudio.blogspot.com/2014/08/snoop-dogg-aigomea-show-akitaka-promota.html
Rapper Snoop Dogg ameingia katika mzozo na promoter wa kisiwa cha
Ibiza ambaye amemfanya kuigomea show aliyokuwa amepanga kuifanya huko
kutokana na kushindwa kukamilisha sharti la kumtumia ndege binafsi.Snoop amepost video kwenye Instagram kuhusu mzozo huo katika kila hatua aliyokuwa anaifanya kuhakikisha anawafikia mashabiki wake wa Ibiza.
Alipost video nyingine akiwa katika uwanja wa ndege wa Vienna, Austria ambapo alidai alikaa kwa muda wa saa 7 bila kutumiwa private jet na promoter huyo.
Baada ya promoter huyo kuendelea kuwa kimya, rapper huyo aliamua kubadili ratiba na kuelekea Belgium kupiga vimeo vyake huku akiwaomba radhi mashabiki wake waliokuwa wanamsubiri.
kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu. LIKE HAPA
